• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Mamia ya wakazi wakosa nafasi za wana wao katika shule za maeneo ya Mukuru

Mamia ya wakazi wakosa nafasi za wana wao katika shule za maeneo ya Mukuru

Na SAMMY KIMATU

MAMIA ya wazazi wanatafuta nafasiza wanao katika shule za umma katika maeneo ya Mukuru katika kaunti ya Nairobi bila mafanikio huku walimu wakuu wakisema shule zimejaa kupita kiasi.

Katika tarafa ya South B shule nne za umma zilizo na udhamini wa kanisa katoliki hazikuweza kuchukua idadi inayoongezeka ya wanafunzi ambao walikuwa wakitarajia kupata nafasi.

Mtawa ambaye hawezi kutajwa kwa sababu ya itifaki alisema kuwa shule nne zilizopo katika eneo hilo zilikuwa na watoto wengi kupita kiasi. Shule hizo ni shule ya Msingi ya St Bakhita, Sancta Maria Mukuru, St Catherine na St Elizabeth ambazo zimedhaminiwa na Sisters of Mercy Kenya Chapter.

“Tuna St Catherine, Sancta Maria Mukuru, na St Bakhita katika maeneo ya South B. Pia tuna shule ya St Elizabeth katika mtaa wa mabanda wa Mukuru- Lunga Lunga lakini watoto ni wengi kuliko madarasa,” alisema mtawa huyo.

Vile vile, katika mtaa wa mabanda wa Mukuru Kwa Njenga katika kaunti ndogo ya Embakasi kuna shule mbili pekee za ummaamabazo ni – Shule ya Our Lady of Nazareth na shule ya Mukuru-Kwa Njenga.

Katika kaunti iyo hiyo, Shule ya Mukuru Reuben Centre na Shule ya Msingi ya Gatoto ndizo shule pekee za umma zinazopatikana lakini haziwezi kutoshea idadi kubwa ya wanafunzi katika mitaa hiyo.

Katika mtaa wa mabanda wa Mukuru-Lunga Lunga katika kaunti ndogo ya Makadara, shule ya msingi ya Star of Hope ndiyo shule pekee ya umma katika eneo hilo nayo pia imejaa.

Kuna ongezeko la idadi ya wanafunzi mwaka huu kwa sababu ya idadi kubwa ya watu katika mitaa ya mabanda ya Nairobi baada ya nyumba nyingi za mabanda kugeuzwa kujengwa za orofa tangu miaka mitatu iliyopita.

Kutokana na Unyakuzi wa ardhi ya umma, hakuna nafasi tupu zilizoachwa hata kwa upanuzi wa shule lakini vyumba vya mikutano, vyoo vya umma na viwanja vya michezo.

  • Tags

You can share this post!

Gor Mahia kujua mpinzani wao kwenye mchujo wa Kombe la...

Mapishi ya samaki aina ya salmon