• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Mjakazi hatari kukaaa rumande siku 5

Mjakazi hatari kukaaa rumande siku 5

Na RICHARD MUNGUTI

MJAKAZI hatari anayedaiwa aliwajeruhi watoto wawili baada ya kutimuliwa kazi na mwajiri  kazi mjini Nairobi atafunguliwa mashtaka ya kujairbu kuua.

Bi Gladys Naliaka Nalianya alifikishwa mbele ya hakimu mkuu Bi Emily Ominde Jumatatu aliamuru azuiliwe rumande kwa wiki moja kuhojiwa.

Bi Ominde aliamuru mjakazi huyo azuiliwe katika kituo cha polisi cha Burburu hadi Machi 22,2021 atakapofikishwa kortini.

Akiwasilisha ombi Bi Naliaka azuiliwe Koplo Josephine Nduku alieleza mahakama mshukiwa alitiwa nguvuni mjini Eldoret akijaribu kutoroka mnamo Machi 13 siku mbili baada ya kuwakata kata kwa upanga watoto wawili wa mwajiri wake Bi Karen Gacheru.

“Nahitaji muda wa siku tano kumhoji mshukiwa huyu kuhusiana shambulizi hilo lilitokea katika mtaa wa Greenfield, Nairobi Machi 11,2021,” Koplo Naliaka alimweleza hakimu.

Mahakama ilielezwa wahasiriwa wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi.

Wahasiriwa walikatwa vichwani na shingoni. Hakimu alielezwa mshukiwa huyo ataulizwa kuonyesha polisi kule alitupa silaha alizotumia kuwajeruhi watoto hao.

Alipoachishwa kazi, mahakama , ilielezwa mjakazi huyo aliapa kuwasababishia maumivu watakayoishi nayo milele.

  • Tags

You can share this post!

Mawakili wamtoroka Sonko tena

Mpangaji taabani kwa kumuua landilodi