• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 10:01 PM
Mke na mwanawe Matasi kufanyiwa upasuaji Jumatatu

Mke na mwanawe Matasi kufanyiwa upasuaji Jumatatu

Na GEOFFREY ANENE

KIPA nambari moja wa zamani wa Harambee Stars, Patrick Matasi amefichua kuwa mkewe na mwanawe wa kiume watafanyiwa upasuaji Juni 7.

Mchezaji huyo wa zamani wa AFC Leopards, Posta Rangers na Tusker, ambaye tangu Oktoba 2018 amekuwa akichezea miamba wa Ethiopia Saint George, alihusika katika ajali mbaya ya barabarani akiwa na familia hiyo yake mnamo Juni 1.

Gurudumu la gari lake lilipasuka gurudumu katika eneo la Lessos mjini Kapsabet katika Kaunti ya Nandi na kubingiria mara kadhaa wakirejea mjini Nairobi kutoka nyumbani katika kaunti ya Kakamega.

Matasi alijeruhiwa kichwani, ingawa alipokea matibabu na kuruhusiwa kuenda nyumbani Juni 4.

Mkewe alivunjika mguu naye mwanawe akaumia mkono.

“Mke wangu na mwanangu watafanyiwa upasuaji mnamo Jumatatu. Mke wangu atawekwa chuma mguuni mwake naye mwanangu atafanyiwa upasuaji wa bega,” kipa huyo mwenye umri wa miaka 33 aliandika kwenye mitandao yake ya kijamii hapo Juni 5.

Matasi, ambaye amechezea Stars mara 26 kati ya Juni 2017 na Kombe la Afrika 2019, ameshukuru Wakenya kwa maombi yao na usaidizi tangu familia hiyo ipate ajali.

“Nashukuru Mungu pia kwa kutuonea huruma,” aliongeza kabla ya kufichua kuwa mwanawe bado hajaimarika, “ingawa yuko chini ya uangalizi wa daktari”.

You can share this post!

TUZO ZA EPL: Beki Ruben Dias na kocha Pep Guardiola waibuka...

Mkenya Brian Mandela asherehekea kushinda Ligi Kuu ya...