• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
Mpenzi ana tabia ya kumezea mate visura waziwazi na kunifanya nihisi sitoshi

Mpenzi ana tabia ya kumezea mate visura waziwazi na kunifanya nihisi sitoshi

SHANGAZI;

Kuna tabia ya mpenzi wangu inayonipa wasiwasi. Anapenda sana kutazama na kutamani wanawake wengine hata tukiwa pamoja. Nimelalamika sana lakini ameshindwa kujirekebisha.

Kuna watu wasiotosheka. Inaonekana hayo ndiyo maumbile ya mpenzi wako na huwezi kumbadilisha. Kama anamezea mate wanawake wengine mkiwa pamoja, atafanya nini akiwa peke yake? Uamuzi ni wako.

Baba mtoto aliniacha sasa nimepata mtu wa kunioa

Mpenzi wangu alitoweka ghafla alipojua nina mimba yake. Alikuwa ameniahidi ndoa. Mtoto wetu sasa ana miaka mitatu na kwa muda wote huo hatujaonana wala kuwasiliana. Kuna mwanamume mwingine anayenipenda na yuko tayari kunioa.

Hali kwamba mpenzi wako alikuacha baada ya kukupa mimba ni ishara hana mapenzi ya dhati kwako. Isitoshe, hajashughulika kujua hali yako na mtoto wenu. Sidhani ana mpango wowote kuhusu maisha yenu pamoja. Msahau na uendelee na maisha yako.

Moyo hautulii, ninashuku ana mpango wa kando

Nina mpenzi ninayemwamini kwa moyo wangu wote. Lakini nimeanza kuona dalili zinazonifanya nishuku ana mwingine. Nashindwa kumuuliza sababu sina ushahidi.

Hujaeleza ni dalili gani umeona ndipo umshuku. Haitakuwa vyema kumkabili kuhusu jambo hilo kwa sababu labda si kweli. Chunguza kwanza uthibitisha.

Nimembania asali akatoa pendekezo la kiajabu

Mpenzi wangu anataka kuonja asali lakini nimemwambia hadi atakaponioa. Anasema hawezi kuvumilia na ameniomba atafute huduma hiyo kwingine tukisubiri ndoa. Ananipenda kweli?

Hayo kamwe si mapenzi. Mwanamume anaongozwa na tamaa. Kwake kukuomba ruhusa ya kutafuta mwingine wa kukidhi tamaa yake ni kukukosea heshima. Mapenzi ya dhati yana subira. Achana naye.

  • Tags

You can share this post!

Azimio sasa washtaki serikali kuhusu mauaji ya...

El Nino itachelewa lakini inakuja, msipuuze, Wakenya...

T L