NA KNA
GAVANA wa Kwale, Bw Salim Mvurya, amehimiza wananchi kutilia maanani viongozi wenye uwezo wa kufadhili sekta ya elimu, katika uchaguzi wa Agosti.
Akizungumza katika mkutano wa umma Ukunda, Bw Mvurya aliambia vijana wachukulie kwa uzito elimu ili kujinufaisha kimaisha.
Alikuwa ameandamana na kamishna wa kaunti hiyo, Bw Gideon Oyagi, ambaye alitaka wananchi watumie nafasi iliyotolewa na serikali kufadhili elimu katika viwango tofauti.