• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 1:42 PM
Mwanamke aliyetishia kudunga kisu mjakazi akishuku anatembea na mumewe kujibu kesi Februari

Mwanamke aliyetishia kudunga kisu mjakazi akishuku anatembea na mumewe kujibu kesi Februari

NA JOSEPH NDUNDA

MWANAMKE mmoja aliyekana tuhuma za kujaribu kumdunga kisu mjakazi wake akimlaumu kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mumewe, atafikishwa mahakamani Februari mwaka ujao.

Leyla Abdikadir aliachiliwa na mahakama ya Makadara kwa dhamana ya Sh200,000 au mdhamini wa Sh100,000 pesa taslim.

Anatuhumiwa kujaribu kumdunga kisu Zuhura Isale nyumbani kwake katika mtaa wa South B, Nairobi mnamo Novemba 11.

Jaribio hilo lilimfanya Bi Isale kuruka dirisha la nyumba hiyo iliyoko orofa ya kwanza akitoroka kabla ya kuanguka kwenye dari.

Mlalamishi huyo bado anapokea matibabu kutokana na majeraha aliyopata wakati wa kisa hicho.

Siku ya tukio hasira za Bi Abdi zilipanda alipompata Bi Isale akimwandalia mumewe staftahi ilhali kanuni iliyoko katika nyumbani hiyo ni kwamba mjakazi hafai kumwandalia mume chakula.

Inadaiwa kuwa mshukiwa alinyanyua kisu na kujaribu kumdunga mlalamishi (Isale) ndiposa akatoroka.

Baada ya kugundua kuwa Bi Isale alijeruhi vibaya, Bi Abdi alimkimbiza katika hospitali ya karibu kabla ya kuhamishwa kwake hadi Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH) kutokana na majeraha mabaya aliyopata.

Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha South B na mshukiwa akasakwa na kukamatwa.

Bi Abdi alikana madai hayo mbele ya Hakimu Mkuu Gerald Mutiso katika Mahakama ya Makadara.

Wakili wake Mbugua Munyiri aliomba mteja wake aachiliwe kwa dhamana nafuu.

  • Tags

You can share this post!

Wetang’ula ataka kaunti zitumie pesa kwa nidhamu ya...

Jinsi Uhuru anavyolenga kupangua mahesabu ya Ruto

T L