NA KENYA NEWS AGENCY
MAHAKAMA ya Narok imemsukuma jela maisha mwanamume mwenye umri wa miaka 50 baada ya kukiri kumnajisi na kumwoa msichana mwenye umri wa miaka 10.
Saigulu Ololosereka aliyefikishwa mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi wa Narok Phyllis Shinyada alikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo kumnajisi msichana wa miaka 10 na kumwoa mnamo 2019.
“Hatia iliyotekelezwa ni hatari na ya kinyama. Miaka mitatu iliyopita ni lazima ilikuwa miaka ya kutisha zaidi kwa mahasiriwa,” alisema Hakimu.