• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 8:50 AM
Nani huyu anakanyaga bibi kichwani, Wakenya wataka kujua

Nani huyu anakanyaga bibi kichwani, Wakenya wataka kujua

NA SAMMY WAWERU

MAPENZI hayana mipaka, na kipendacho roho hula nyama mbichi. Mapenzi pia kikohozi, hayafichiki.

Isemwavyo, mapenzi ni matamu na pia yana gharama.

Lakini yote hayo si hoja, ila sarakasi zingine wanazofanya walio katika bahari ya mapenzi ni za kuajabisha.

Ni kwa mintaarafu hii basi ambapo picha ya mwanamume anayeonekana kumwekea mke wake mguu kichwani imeduwaza wengi.

Jamaa na mke wake wakifurahia miadi. Picha|Hisani

Hata ingawa wanandoa hao hawajambulika wanakotoka, wawili hao wanaonekana walikuwa katika miadi (picnic).

Katika mazingira ya kijani, mke wa jamaa huyo ameegemea kwenye mwamba – jiwe.

Mume naye amelikwea, mguu wa kushoto akiuwekelea kwenye kichwa cha mama wa boma.

Huku wengi wakitamani kukutana nao, Alhamisi picha hiyo iligeuka kuwa gumzo Facebook baada ya ukurasa wa Cops Kenya ambao kulingana na machapisho yake ni wa kuelezea masuala ya maafisa wa usalama nchini, kuipakia.

Baadhi ya wafuasi walijikuna kichwa, wakijaribu kupendekeza eneo wanalotoka wawili hao.

“Nani huyu anakanyaga mama kichwa?” Cops Kenya ikaandika.

Swali hilo aidha liliandaa jukwaa la wanamitandao, majibu ya pozi jamaa na kipenzi chake yakivunja mbavu.

“Live from Keroka, (Moja kwa moja kutoka Keroka,” Evans Maestro KE, akatania.

Keroka ni mojawapo ya mji mkuu Kaunti ya Nyamira.

“Una jawabu,  kwa nini unaulizia?  aki Wakisii mtatuonyesha mambo ,” Nzavi EM Steve kachangia.

“Ni mubaba,” akaandika Njeri Wamiti.

Huku wapekuzi na ‘makachero’ wa mitandao ya kijamii, wakiendeleza oparesheni kutambua majina yao na waliko, baadhi ya sarakasi za aina hiyo zimevunia wahusika sifa.

Wengine, wamejipata kuwa ‘mabalozi’ wa kampuni na mashirika kuhamasisha biashara yao.

Isitoshe, kampuni zinazotoa huduma za utalii hutumia mwanya huo kuwapeleka likizo kujiburudisha.

  • Tags

You can share this post!

Barcelona na Man-United nguvu sawa katika mkondo wa kwanza...

Pasta afariki akiwa kwa mfungo bila maji, chakula kama Yesu

T L