• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Nashindwa kumsaidia mwanamume mpenzi wangu kifedha kwa sababu naona atakataa

Nashindwa kumsaidia mwanamume mpenzi wangu kifedha kwa sababu naona atakataa

SHANGAZI;

Mpenzi wangu hana kazi kwa sasa na ninajua ana shida ya pesa. Nataka kumsaidia lakini nashindwa kumwambia kwa sababu kuna wanaume wasiopenda msaada wa aina hiyo kutoka kwa wanawake. Nahitaji ushauri wako.

Mawazo yako ni ishara ya mapenzi ya dhati. Hata kama hatakubali msaada wako, ni muhimu sana ajue kwamba unaelewa hali yake, unamjali na uko tayari kumsaidia. Mwelezee nia yako.

Kazi ya chumbani siiwezi baada ya kufutwa

Niliachishwa kazi ghafla mwezi uliopita. Ni pigo kubwa kwangu kwa sababu nina mke na watoto wawili. Hali hiyo imeathiri shughuli chumbani na mke wangu anashuku ninatembea nje. Nifanyeje?

Unahitaji msaada wa mke wako kukabiliana na hali hiyo. Mwambie ukweli ili ajue kiini cha upungufu wako chumbani. Jaribu pia kuzungumza na marafiki zako wa karibu ili wakupe mwelekeo.

Mama ataka niishi jijini na baba wa kambo, nahofia

Nilimaliza masomo ya chuo kikuu majuzi. Mama yangu anapendekeza niende mjini nikaishi na baba yangu nikitafuta kazi. Nina wasiwasi kwa sababa huyo si baba yangu mzazi. Naomba ushauri wako.

Kinga ni bora kuliko tiba. Ni hatari kwako kulala nyumba moja na mtu kama huyo. Kama kumekuwa na visa vya baba wazazi kuwatendea maovu binti zao, itakuwaje kwa baba wa kambo? Mwelezee mama yako hofu yako.

Miezi 6 ya uchumba na bado anasema hayuko tayari tufunge ndoa

Nimekuwa na mpenzi kwa miezi sita na nimeamua kumuoa. Nimemwambia lakini anasema hayuko tayari ingawa anasisitiza kuwa ananipenda. Nimechanganyikiwa, nishauri.

Maana ya uchumba ni kwa wahusika kufahamiana vyema kabla ya kufunga ndoa. Miezi sita ya uchumba ni muda mfupi. Mwenzako amekuhakikishia anakupenda, mpe muda.

  • Tags

You can share this post!

Walimu wa shule za msingi wafungiwa nje kusimamia KCSE

Makanisa 20 yaandaa maombi ‘kutakasa’ eneo la Turkwel...

T L