Na SAMMY KIMATU
POLISI wameimarisha doria katika maeneo matatu hatari kwa usalama katika kaunti ndogo ya Starehe, Nairobi.
Akizungumza na Taifa Leo jana Jumanne, mkuu wa polisi eneo la Makadara, Bw Timon Odingo, alisema serikali ilichukua hatua baada ya kupokea malalamishi ya wananchi.
Maeneo hayo ni pamoja na steji ya matatu za South B, barabara ya Bunyala, kutoka uga wa Nyayo kuelekea steji ya Bellevue na daraja la barabara ya Likoni eneo la viwandani.