Na WAIKWA MAINA
GAVANA wa Nyandarua Francis Kimemia, anakabiliwa na wakati mgumu akijiandaa kutetea kiti chake kwenye uchaguzi mkuu ujao huku washirika wake wakijitenga naye.
Bw Kimemia amekuwa akikosolewa vikali na Mwakilishi wa Wanawake, Bi Faith Gitau na Waziri wa Maji, Bi Sicily Kariuki anayemezea mate kiti cha ugavana Kaunti ya Nyandarua.