NA VITALIS KIMUTAI
POLISI na maafisa wa utawala kutoka Kaunti ya Bomet mnamo Jumanne, Desemba 26, 2023 walinasa misokoto ya bangi inayokadiriwa kuwa ya thamani ya Sh342,000.
Mshukiwa mmoja alikamatwa akiwa na misokoto hiyo. Chifu wa Lokesheni ya Kyogong, Selina Kilel alisema mshukiwa huyo alinyakwa kufuatia habari kutoka kwa umma.
“Mshukiwa alikamatwa katika kijiji cha Chepkusui akiwa na misokoto 341 ya bangi kutokana na oparesheni iliyoendeshwa mnamo Jumanne,” akasema Bi Kilel.
Mshukiwa huyo alifikishwa katika kituo cha polisi cha Bomet na anatarajiwa kufikishwa kortini.
Hali ya usalama nchini imeimarishwa kabla, wakati na baada ya sherehe za Krismasi 2023.