• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Polisi waokoa msichana aliyetaka kujitia kitanzi kwa kutumia kijivazi cha ndani

Polisi waokoa msichana aliyetaka kujitia kitanzi kwa kutumia kijivazi cha ndani

NA EVANS JAOLA

[email protected]

POLISI mjini Kitale wamemuokoa msichana tineja aliyetaka kujitia kitanzi ndani ya seli akitumia kivazi chake cha ndani.

Msichana huyo alikuwa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Sirende kaunti ndogo ya Kiminini pamoja na mwenzake ambaye wamepitana mwaka mmoja tu kwa umri.

Wasichana hao wote wawili walikuwa na makosa ya kutoroka nyumbani kuenda kwa wapenzi wao wa kiume.

Wazazi wao waliripoti polisi walipokuwa wametoweka. Wazazi walitaka wasichana hao wazuiliwe ili wataje wanaume waliowanyanyasa kimapenzi ikizingatiwa kwamba ni wasichana ambao hawajagonga umri wa kuingia utu uzima, miaka 18.

Ripoti ya daktari ilisema msichana aliyetaka kujitia kitanzi alikuwa mjamzito na yule mwenzake alikuwa amevunjwa ubikira japo hakuwa mjamzito.

Polisi wameeleza wanahabari kwamba msichana huyo aliyejaribu kujitia kitanzi alifunga kivazi hicho cha ndani kwa shingo na kufunga kwa mlango wa seli ya polisi.

Mwenzake alivyoona hatari iliyokuwa ikimkodolea, alipiga usiahi kuita polisi kumuokoa.

Alipelekwa kwa hospitali ya St John’s Sirende Mission akapewa huduma ya kwanza kabla ya kuhamishiwa hadi katika hospitali ya Kitale ambapo anaendelea kupata nafuu.

Afisa wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Francis Kihara amesema maafisa wanafanya uchunguzi kuwakamata wanaume waliotenda makosa hayo ya kuharibu watoto wadogo ili wafunguliwe mashtaka.

  • Tags

You can share this post!

Siasa ilibonda vibaya mifuko yangu, akiri mcheshi MC Jessy

Kipusa Ntalami ashtaki kipindi cha televisheni kutumia...

T L