• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
Kipusa Ntalami ashtaki kipindi cha televisheni kutumia picha zake bila idhini

Kipusa Ntalami ashtaki kipindi cha televisheni kutumia picha zake bila idhini

Na FRIDAH OKACHI

Mfanyabiashara na soshiolaiti Michelle Ntalami ameishtaki kampuni ya Mnet pamoja na mwigizaji Minne Kariuki kutokana na kutumia picha yake bila idhini yake. 

Michelle Ntalami ni mkurugenzi mtendaji wa bidhaa za Marini Naturals. Ntalami amechukua hatua hiyo baada ya picha yake kutumika kwenye kipindi cha The Real Housewives of Nairobi.

Ntalami anadai kuwa wakati wa kuchuliwa kwa picha hizo, hakuwa miongoni mwa wale waliokuwa wameteuliwa kwenye kipindi hicho bali alikuwa mgeni wa Susan Kaitanny kwenye sherehe iliyokuwa ikiendelea katika mkahawa wa Triple Hotel November 22, 2022.

Mawakili wa Ntalami, kutoka kampuni ya Kilonzo & Company Advocates wamemtaja mwigizaji Minne Kariuki, televisheni ya Young Rich, M-NET na D&R Studios limited kuwa washtakiwa katika barua iliyoandikwa Septemba 25, 2023.

Televisheni ya Young Rich, M-NET na D&R Studios Limited imeshtakiwa kwa kusambaza picha na sauti kwenye mitandao yao ya kijamii.

Minnie Kariuki akishtakiwa kwa kumdhuru kwa kuchapisha habari za uongo kupitia mitandao ya kijamii na kukiuka sheria ya Faragha na data.

Ntalami anataka mahakama iweze kuwaelekeza washtakiwa hao kuondoa picha na sauti yake iliyotumika kwenye vipindi vyote.

Pili akitaka mshtakiwa wa kwanza kwa jina Minnie Kariuki, kuomba msamaha wa lazima kwa kusababisha dhuluma baada ya kuchapisha habari za uongo kwenye mitandao ya kijamii na kumchafulia sifa.

Ntalami aliongezea kuwa maneno yaliyoandikwa naye Minnie Kariuki, yalikuwa yenye uongo mtupu.

Kulingana na uchapishaji wa picha na sauti zake zilizotumika, zimemsababishia Ntalami kuwa na matatizo ya kiakili kutokana na dhuluma aliyoipata, wanadai mawakili wake.

“Kuna jambo kuhusu watu wazuri. Wanakupa nafasi kwa neema. Leo nachukua msimamo thabiti kwa ajili yangu na wanawake wengine dhidi ya kudharauliwa na kudhalilishwa kupitia video moja ya The Real Housewife of Nairobi. Ni aibu kujua kwamba wasimamizi wa kipindi hiki wanawatumia wengine visivyo. Inaathiri afya ya akili na ustawi wa mtu binafsi kwa kukiuka sheria za utangazaji hapa nchini,” aliandika Ntalami kwenye ukurasa wa Instagram.

  • Tags

You can share this post!

Polisi waokoa msichana aliyetaka kujitia kitanzi kwa...

Nashindwa kuambia mke wangu dadake ni mkora, huenda...

T L