• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Raila, Gachagua wachomeana picha mazishini

Raila, Gachagua wachomeana picha mazishini

NA WINNIE ONYANDO

NAIBU Rais Rigathi Gachagua na Kiongozi wa Azimio Raila Odinga wamechomeana picha Ijumaa katika mazishi ya shujaa wa Mau Mau, John Kagwe almaarufu Brigedia Kiboko eneo la Ngorika, Kaunti ya Nyandarua.

Wawili hao wamerushiana maneno huku kila mmoja akijaribu kumpaka mwenzake tope.

Bw Gachagua amedai kuwa Bw Odinga alimvuruga Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, jambo analosema limemfanya achukie handisheki.

“Nakuambia leo ukiwa hapa, tunaogopa sana handisheki. Ushirikiano wako na Uhuru ulitutia hofu. Akiwa na wewe anacheka, akija hapa amekasirika. Hii ndio maana hatutaki handisheki,” Gachagua akasema huku waliohudhuria mazishi wakiangua kicheko.

Kadhalika, Bw Gachagua amedai kuwa Rais Mstaafu aliacha kujihusisha sana na mambo ya dini kwa sababu ya Bw Odinga.

“Uhuru alikuwa anapenda sana mambo ya kanisa lakini akabadilika pindi tu alipoanza kushirikiana nawe,” akaongeza Bw Gachagua.

Kwa upande wake, Bw Odinga amedai kuwa ni yeye alimlipia shujaa wa Maumau bili ya hospitali kwa sababu familia haikuweza kumfikia Bw Gachagua.

“Nilimwambia daktari wangu apige simu ili wamlaze mzee huyo. Hii ilikuwa baada ya familia kujaribu kumfikia Bw Gachagua bila mafanikio,” akasema Bw Odinga.

  • Tags

You can share this post!

KCB wapata wanyonge droo ya Tisap Sevens

Mudavadi aitaka KRA iibuke na mbinu bora za ukusanyaji...

T L