• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
Mudavadi aitaka KRA iibuke na mbinu bora za ukusanyaji ushuru

Mudavadi aitaka KRA iibuke na mbinu bora za ukusanyaji ushuru

NA WINNIE ONYANDO

KINARA wa Mawaziri Musalia Mudavadi ametoa wito kwa Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru nchini (KRA) kubuni mbinu za kuboresha ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza Ijumaa mjini Eldoret, ambapo aliongoza hafla ya kufuzu kwa maafisa 1,405 wasaidizi wa ukusanyaji ushuru nchini (RSAs), Mudavadi alisema mapato yanaweza yakaongezeka ikiwa KRA itatumia mbinu bora kuwarai walipa ushuru kutekeleza wajibu wao.

Hata hivyo, alisema kuwa kwa sasa serikali imeanzisha mchakato wa kubadilisha usimamizi wa KRA, hatua aliyosema inalenga kuiwezesha serikali kufikia lengo lake la kukusanya ushuru wa ziada.

Alisema KRA inafaa kila wakati kukumbatia weledi na kuimarisha utendakazi wake na pia kudumisha haki.

“Ni wajibu wa Wakenya kushirikiana na KRA ili kurahisisha ukusanyaji wa ushuru,” akasema Bw Mudavadi.

Kwa sasa Kamishna Mkuu wa KRA ni Humphrey Wattanga Mulongo aliyeanza kazi wiki hii.

  • Tags

You can share this post!

Raila, Gachagua wachomeana picha mazishini

Jinamizi la ahadi Ruto akizuru Magharibi

T L