• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:55 AM
Seneta Mithika Linturi ashtakiwa kwa dhuluma za kimapenzi

Seneta Mithika Linturi ashtakiwa kwa dhuluma za kimapenzi

Na RICHARD MUNGUTI

SENETA wa Meru Mithika Linturi Jumanne alishtakiwa kwa kumdhulumu mwanamke kimapenzi kwa kushika nyeti zake na matiti.

Mbali na shtaka hilo la kumshushia heshima mwanamke huyo aliye na umri wa miaka 36 , Bw Linturi alishtakiwa kwa kosa la kujaribu kumbaka.Endapo atapatikana na hatia Bw Linturi atasukumwa jela miaka mitano ama kifungo cha maisha kwa kujaribu kumbaka mwanamke huyo katika hoteli moja mjini Nanyuki kaunti ya Laikipia

Kushtakiwa kwa Bw Linturi mbele ya hakimu mwandamizi Bi Martha Nanzushi katika mahakama ya Milimani kulifuatia kukataliwa kwa ombi la kuzima kushtakiwa kwake.

Bw Linturi aliwasilisha ombi katika mahakama  akipinga hatua ya mkurugenzi wa uchunguzi wa jinai na mkurugenzi wa mashtaka ya umma kumfungulia mashtaka ya dhuluma za kimapenzi.

Bw Linturi alikanusha mashtaka  yote mawili kisha mawakili wake Mabw Charles Mwongera, Gitobu Imanyara, Muthomi Thiankolu na Margaret Ngesa waliomba aachiliwe kwa dhamana wakisema “ni seneta na hawezi toroka.”

Upande wa mashtaka uliongozwa na Bi Everlyne Onunga ambaye alisema hapingi mshtakiwa akiachiliwa kwa dhamana.“Sipingi mshtakiwa akiachiliwa kwa dhamana ila ninaomba hii mahakama imwamuru asiwavuruge mashahidi kwa njia yoyote ile,” Bi Onunga alieleza mahakama.

Bw Mwongela alieleza mahakama mshtakiwa atatii masharti ya mahakama.Bi Nanzushi alimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya pesa tasilimu Sh200,000 na kumwagiza asithubutu kuwavuruga mashahidi kwa njia yoyote ile.

Bw Linturi alikabiliwa na shtaka kuwa mnamo Januari 30, 2021 katika Hoteli ya Maiyan Villas Hotel mjini Nanyuki alijaribu kumbaka mwanamke.Pia alikana shtaka la kumdhulumu mlalamishi huyo anayewakilishwa na Bw Ben Nzakyo matiti na sehemu zake nyeti bila idhini yake.

  • Tags

You can share this post!

Salah afikisha mabao 100 ya EPL baada ya kusakata jumla ya...

Griezmann ashindwa kung’aa katika mechi ya kwanza ya...