• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 3:10 PM
Ujerumani kuvaana na Uingereza kwenye hatua ya 16-bora ya Euro

Ujerumani kuvaana na Uingereza kwenye hatua ya 16-bora ya Euro

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

UJERUMANI watakutana sasa na Uingereza kwenye hatua ya 16-bora ya Euro baada ya kutoka nyuma mara mbili na kusajili sare ya 2-2 iliyowabandua Hungary.

Adam Szalai anayechezea Mainz ya Ujerumani aliwaweka Hungary kifua mbele jijini Munich. Andras Schafer alidhani alikuwa amefungia Hungary bao la ushindi sekunde 90 baada ya Kai Havertz kusawazishia Ujerumani.

Hata hivyo, masogora wa kocha Joachim Loew walisawazisha kupitia Leon Goretzka mwishoni mwa kipindi cha pili.Matokeo hayo yanamaanisha kwamba Ujerumani kwa walikamilisha kampeni za Kundi F katika nafasi ya pili na watakutana na Three Lions wa Uingereza mnamo Juni 29 uwanjani Wembley.

Mechi kati ya Ujerumani na Uingereza itarejesha kumbukumbu za Euro 1996 ambapo vikosi hivyo vilikutana kwenye nusu-fainali. Ujerumani ambao ni mabingwa mara nne wa dunia waliibuka washindi kupitia mikwaju ya penalti.

 

  • Tags

You can share this post!

Man-United kuvunja benki kwa ajili ya Sancho

Ujerumani kuonana na Uingereza huku Ureno wakipepetana na...