NA JOHN ASHIHUNDU
Wachezaji wa AFC Leopards wamekataa kufanya mazoezi hadi walipwe mshahara wao wa miezi miwili.
Vijana hao wamepangiwa kucheza na Bandari leo ugani Nyayo, lakini wameamua kuendelea na mgomo huo tangu Alhamisi.
Wiki chache zilizopita, klabu hiyo ilitangaza kuwa na matatizo ya kifedha huku ikiomba Kaunti ya Kakamega iingilie kuokoa jahazi, lakini haikufanikiwa katika maombi hayo yaliyowasilishwa na mwenyekiti Dan Shikanda.
Kabla ya kuanza mgomo huo, wachezaji walieleza jinsi wanavyoteseka pamoja na jamii zao zinazowategemea.
Wakati Leopards wakiendelea kukumbwa na shida hiyo, maadau wao wakuu Gor Mahia pia wanasemekana kuwa na matatizo kama hayo, na huenda mashabiki wao wakashuhudia mgomo kwa musa usio mrefu.