• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:12 PM
Walioachiliwa kuhusiana na mauaji ya dereva wa teksi Kericho wasakwa tena

Walioachiliwa kuhusiana na mauaji ya dereva wa teksi Kericho wasakwa tena

Na FRIDAH OKACHI

POLISI katika Kaunti ya Uasin Gishu wanawasaka washukiwa wawili wa mauaji ya dereva wa teksi ambao walikuwa wameachiliwa na mahakama kwa ukosefu wa ushahidi.

Naibu Kamanda wa polisi katika Kaunti Ndogo ya Ainabkoi Alois Muthoka, alisema watafunguliwa mashtaka mapya ya mauaji na wizi wa kimabavu.

“Mwili wa dereva wa teksi John Muiruri Ndungu ulipatikana katika shamba la kawaha Kaunti ya Kericho katika eneo la Chepsinoi. Wanaume hao wawili ambao walikuwa wameachiliwa watakamatwa na kuzuiliwa kwa uchunguzi mpya,”alisema Bw Muthoka.

Mke wa marehemu Grace Muiruri, ameomba maafisa wa polisi na mahakama kuhakikisha familia yake inapata haki. Bi Muiruri alisema mumewe  ndiye aliyekuwa tegemeo lao.

“Naomba mahakama inifanyie haki, nina watoto wanne. Watatu wanasoma vyuo vikuu na kifunga mimba ni mdogo yuko shule ya chekechea,”alisema Bi Muiruri.

Hatua hiyo inajiri huku wahudumu wa teksi mjini Eldoret Kaunti Uasin Gishu na Mwakilishi wadi ya Langas Francis Muya wakilaani kitendo hicho.

Wahudumu hao wanapanga kufanya maandamano ya amani kushinikiza uimarishaji wa usalama.

Mwili wa dereva wa teksi John Muiruri Ndungu ulipatikana ametupwa katika shamba la kahawa Kaunti ya Kericho eneo la Chepsinoi baada ya kutoweka Oktoba 14, 2023.

Juma lililopita, polisi wa Kapsoya Kaunti ya Uasin Gishu walikamata genge la watu watano waliopatikana wakihusika na biashara ya wizi wa magari.

  • Tags

You can share this post!

Wanamapinduzi Niger wadai wamezima jaribio la Rais Bazoum...

Wauguzi 66 watuzwa kwa kazi nzuri ya kuwashughulikia...

T L