• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 2:11 PM
Waliompora mwanafunzi washtakiwa

Waliompora mwanafunzi washtakiwa

Na RICHARD MUNGUTI

WASHUKIWA wawili wa ujambazi waliokamatwa na simu na bidhaa walizomnyang’anya mwanafunzi wa chuo kikuu wameshtakiwa kwa wizi wa mabavu.

Wawili hao Shandrack Kimanzi na Mwalimu Hamisi walikanusha shtaka la kumnyang’anya kwa nguvu  Bi Valary Mukhebi simu, bidhaa alizokuwa amenunua Supa kabla ya kutoroka.Walimkabili Bi Mukhebi mwanafunzi wa chuo kikuu cha Tanganza alipokuwa akienda katika cha malazi eneo la Karen katika barabara ya Langata  Nairobi.

Washtakiwa hao walipomkabili Mukhembi walimtisha asipige duru ama aone cha mtema kuni.Mmoja aliponyoka na mkoba wake uliokuwa na simu na mwingine akachana mbuga akiwa na bidhaa za matumizi mlalamishi alizokuwa amenunua supa.

Mlalamishi alipiga kamsa kisha wanaboda boda wakawafukuza kisha wakawapokonya washtakiwa bidhaa walizokuwa wamemnyang’anya mwanafunzi huyo.Hakimu mwandamizi Bw Peter Mutua alielezwa washtakiwa hao walikutwa na simu, sabuni na mafuta ya kujipondoa yenye thamani ya Sh1,450 na simu iliyo na thamani ya Sh11,000.

Washtakiwa walikana mashtaka na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh300,000 kila mmoja.

  • Tags

You can share this post!

Asukumwa jela miaka miwili kwa kupatikana na pingu

Mwanamke ashtakiwa kumdhulumu bintiye