• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Wanaume wawili wananitaka, sijui nichague yupi kati yao; ninawapenda wote

Wanaume wawili wananitaka, sijui nichague yupi kati yao; ninawapenda wote

SHANGAZI;

Kuna wanaume wawili wanaonitaka kimapenzi. Nimechanganyikiwa kwa sababu kuna mambo tofauti ninayopenda kwa kila mmoja wao. Nataka kuolewa nitulie maishani. Nifanyeje?

Naelewa kuwa unawapenda wote wawili ndiposa umeshindwa kuchagua mmoja. Kwa kuwa unasema wakati wako wa kuolewa umefika, itabidi ufunge macho uchague mmoja ndipo utimize lengo lako.

Demu ni mbishani ajabu, itakuwaje ndoa?

Nina mpenzi ninayependa kwa dhati. Tatizo ni kuwa anapenda ubishi sana na pia haniheshimu hata mbele ya watu. Ningependa kumuoa lakini tabia yake hiyo inanitia hofu.

Kuna watu wenye tabia za kimaumbile na ni vigumu kuwarekebisha. Ubishi na dharau huzaa ugomvi, ambao ni sumu katika ndoa. Kama hutaki maisha ya ugomvi, achana na mwanamke huyo.

Aliyenasa moyo wangu kumbe ni demu wa rafiki

Juzi nilikutana na mwanamke fulani aliyenasa moyo wangu. Nilimwambia na akaomba muda afikirie. Sasa nimegundua kwamba yeye ni mpenzi wa rafiki yangu.

Hali kwamba mwanamke huyo hakukwambia wazi ana mpenzi ni ishara hana uhakika na uhusiano huo. Akiamua kumuacha kwa ajili yako ni sawa. Lakini pia kuwa tayari kumpoteza rafiki yako.

Shangazi, ninakutaka wewe uwe mpenzi

Sina mke wala mpenzi ingawa nina miaka 45. Nimechelewa kuoa kwa sababu natafuta mwanamke stadi wa mapenzi na mwenye ujuzi kuhusu ndoa. Moyo wangu umetua kwako. Wasemaje?

Kwanza, ondoa kabisa mawazo yako kwangu. Mimi nishapata wangu ambaye ananitosha. Pili, mwanamke ambaye hajaolewa hawezi kuwa na ujuzi wowote kuhusu ndoa, kwa sababu bado hajaolewa! Lakini stadi wa mapenzi wako tele. Fungua macho na utamuona.

  • Tags

You can share this post!

Kabura kujitetea katika kesi ya uporaji wa Sh791 milioni za...

Shule yatoa ilani kuhusu apu ya Roblox inayoweka watoto...

T L