• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Wawili washtakiwa kudandia meli iliyobeba mibuyu kuelekea Georgia

Wawili washtakiwa kudandia meli iliyobeba mibuyu kuelekea Georgia

NA BRIAN OCHARO

WATU wawili wameshtaki wa kwa kuingia kwa njia haramu kwenye meli ya mizigo iliyokuwa inabeba miti ya mbuyu kwenda Georgia.

Ali Mbaraka na Hassan Ali walifikishwa mbele ya mahakama ya Mombasa jana kwa tuhuma za kushindwa kuripoti kuondoka kwao wakiwa kwenye meli hiyo kwa afisa wa uhamiaji aliye karibu.

Mashtaka yanaonyesha wawili hao walipatikana wakiwa wamejificha ndani ya MV RIVER MAS mlikokuwa miti hadi walipogunduliwa siku mbili kabla ya meli hiyo kuondoka kutoka bandari ya Mombasa.

Washukiwa hao pia walifunguliwa mashtaka kwa kosa la kuingia katika meli hiyo bila idhini.

Washukiwa hao walikiri makosa hayo walipofikishwa mbele ya Hakimu wa Mombasa Vincent Adet.

Waliiomba mahakama kuwaonea huruma wakisema familia zao zinawategemea.

Serikali ilisema washukiwa walitenda makosa hayo Agosti 24, katika Bandari ya Mombasa.

Washukiwa wamezuiliwa rumande wakisubiri hukumu.


  • Tags

You can share this post!

Ukaguzi: Kaunti ya Homabay imejaa wafanyakazi hewa, wengine...

Kenya yaambulia patupu marathon ya wanawake jijini Budapest

T L