NA KNA
WAKAZI katika Kaunti ya Taita Taveta, wamelalamikia hali mbaya ya uwanja wa michezo wa Moi ambapo inadaiwa sasa umegeuzwa kuwa danguro na watu wasioweza kulipia gesti.
Ujenzi wa uwanja huo umekuwa ukitatizwa na madai ya ufisadi katika miaka iliyopita.
Waziri wa Vijana, Utamaduni na Michezo katika kaunti, Bw Shedrack Mutungi, alisema serikali ya Gavana Andrew Mwadime, inatambua hali mbaya ya uwanja huo na tayari kuna mipango ya kufanya ukarabati.
Bw Mutungi alisema, wamepanga kukutana na Waziri wa Michezo, Bw Ababu Namwamba, ili kuona kama serikali ya kitaifa inaweza kusaidia kuukarabati.
Uwanja huo pia umesemekana kutumiwa kama makazi ya familia za kurandaranda mitaani, huku pia malori na mabasi yakiegeshwa hapo.