NA ALEX NJERU GAVANA
MUTHOMI Njuki amekashifu baadhi ya viongozi wa Tharaka Nithi ambao wamekosoa rekodi yake ya maendeleo.
Akizungumza alipokuwa akizindua daraja linalounganisha wadi ya Mariani na Mitheru jana, Bw Njuki aliwaomba wanasiasa hao kumpa muda wa kutekeleza manifesto yake.
“Nina mpango wa maendeleo na hakuna kiasi cha kelele kutoka kwa wanasiasa kitakachoniyumbisha kutoka kwa mpango wangu kwa miaka mitano ijayo,” gavana aliwaambia wakazi.