Na DERICK LUVEGA
GAVANA wa Kaunti ya Vihiga, Wilber Ottichilo, amepata pigo baada ya juhudi zake za kuzuia kesi ya kudharau mahakama inayomkabili, kutupiliwa mbali na Mahakama Kuu.
Kesi hiyo iliwasilishwa na maafisa wakuu wa serikali ya kaunti aliowafuta kazi mwezi Juni.
Mahakama iliagiza warudishwe kazini lakini Dkt Ottichilo alijaza nafasi zao.