Na BONFACE OTIENO
ABIRIA wanaosafiri kutoka Mombasa hadi Kisumu, wataanza kutumia gari moshi usiku na mchana mwezi ujao, baada ya reli ya kisasa (SGR) kuunganishwa na ya zamani iliyokarabatiwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli la Kenya (KRC), Bw Philip Mainga, alisema hatua itawafaidi abiria watakaosafiri mashambani magharibi mwa Kenya na Nyanza ingawa hakutaja tarehe rasmi ya kuanza.