Na WYCLIFFE NYABERI
WAKFU wa Aga Khan, umetoa msaada wa vifaa vya kujikinga dhidi ya corona kwa kaunti tano.
Kwa ushirikiano na Mataifa ya Muungano wa Ulaya (EU) na hospitali ya Aga Khan Kisumu, vifaa hivyo vyenye thamani ya Sh 13.5 milioni, vitafaidi hospitali katika kaunti za Kisii, Migori, Kisumu, Bungoma na Busia.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Hospitali ya Aga Khan Kisumu, Bi Jane Wanyama, alisema mpango unalenga kukabili corona.