• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Shirika la Reli kuongeza safari za treni Kisumu

Shirika la Reli kuongeza safari za treni Kisumu

VICTOR RABALLA NA RUSHDIE OUDIA

SHIRIKA la Reli la Kenya kesho Ijumaa litaanzisha safari za treni usiku kati ya Nairobi na Kisumu.

Treni hiyo itakuwa ikiondoka Nairobi na Kisumu saa kumi na mbili unusu jioni kila Ijumaa na Jumapili na kuwasili saa kumi na mbili asubuhi.

Kulingana na ratiba ya shirika hilo, wasafiri watalipa nauli ya Sh600 kutoka Nairobi hadi Kisumu, Sh300 kati ya Nairobi na Nakuru na Sh400 kutoka Nakuru hadi Kisumu huku wale watakaosafiri katika kitengo maalumu wakilipa Sh2,000.

Wanaosafiri katika kitengo maalum watapata huduma za Wi-Fi, vinywaji na mahali pa kuweka mizigo yao.

Shirika hilo lilianzisha huduma kati ya Nairobi na Kisumu mnamo Desemba 17 baada ya kuzisimamisha kwa zaidi ya miaka 10.

  • Tags

You can share this post!

ZARAA: Afichua siri ya jinsi alivyofaulu katika kilimo cha...

Maoni yaweka Raila hatua kadhaa mbele ya Ruto

T L