• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 5:50 AM
Kampuni ya maji yashtakiwa kwa kuhatarisha afya

Kampuni ya maji yashtakiwa kwa kuhatarisha afya

Na GEORGE ODIWUOR

WANAHARAKATI wawili wameishtaki Kampuni ya Maji na Usafishaji ya Kaunti ya Homa Bay kwa kuhatarisha afya ya watu baada ya kuachilia maji machafu kutoka kwa kiwanda cha majitaka mjini humo.

Wawili hao walifika kortini kupinga hatua ya kampuni hiyo ya kuachilia maji kutoka kijiji cha Arunda.

Licha ya maji hayo kuwa machafu, huwa yanaachiliwa katika makazi ya watu kabla ya kutumiwa na binadamu na mifugo.

Kesi hiyo imewasilishwa katika mahakama ya ardhi na mazingira.

  • Tags

You can share this post!

Walanguzi 3 wa dawa za kulevya wakamatwa

Wabunge Homa Bay waingia boksi ya Gavana Wanga

T L