• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Lempurkel ashtakiwa upya kwa matamshi ya uchochezi

Lempurkel ashtakiwa upya kwa matamshi ya uchochezi

Na RICHARD MUNGUTI

ALIYEKUWA mbunge wa Laikipia Kaskazini Bw Mathew Lempurkel alishtakiwa upya Januari 13, 2022 kwa matamshi ya uchochezi.

Bw Lempurkel aliyewakilishwa na Bw Saitabai ole Kanchory alikana shtaka la kuchochea hisia za chuki dhidi ya watu wenye mashamba makubwa katika kaunti ya Laikipia.

Bw Lempurkel anadaiwa alitoa matamshi hayo wakati wa mahojiano na kituo cha televisheni cha Maa TV mnamo Julai 17, 2021.

Shtaka hilo lilidai matamshi hayo yalilenga kuibua hisia za chuki dhidi ya wamiliki wa mashamba makubwa.

Bw Lempurkel alikana shtaka hilo mbele ya hakimu mwandamizi katika mahakama ya Milimani Bw Bernard Ochoi.

Bw Kanchory aliomba mahakama iamuru dhamana aliyopewa mshtakiwa mwaka 2021 imgharimie mshtakiwa sasa.

Bw Ochoi aliamuru dhamana aliyolipa mshtakiwa mwaka 2021 imsimamie.

Kesi hiyo itatajwa tena Februari 16, 2022 kwa maagizo zaidi.

  • Tags

You can share this post!

UJAUZITO NA UZAZI: Kuongeza madini ya chuma mwilini

Raila adai Ruto alichangia kufeli kwa Jubilee

T L