• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Mwalimu asakwa akidaiwa kuwaua kwa kuwachinja wanawe wawili

Mwalimu asakwa akidaiwa kuwaua kwa kuwachinja wanawe wawili

NA MWANGI MUIRURI

POLISI katika Kaunti ya Murang’a wanamsaka mwalimu mmoja wa kiume wa Shule ya Upili ya Kamacharia mwenye umri wa miaka 33 baada ya kushukiwa kuwaua watoto wake wawili kwa kuwachinja shingoni kwa kisu.

Mwalimu huyo kwa jina James Gitau Karanja, yuko mafichoni huku makachero wakimsaka baada ya miili ya Roy Irungu aliyekumbana na mauti akiwa na umri wa miaka mitano na Joseph Karanja wa umri wa miaka miwili na nusu kupatikana nyumbani kwake katika kijiji cha Kieni kilichoko eneobunge la Kiharu wakiwa wamelala kwa damu yao kitandani.

Seneta wa Murang’a Bw Joe Nyutu ameyataja mauaji hayo kuwa ni unyama na kitendo cha kishetani ambacho hakifai kamwe.

Kamanda wa Polisi wa Murang’a Bw Mathiu Kainga alisema kwamba tayari miili ya watoto hao imepelekwa katika mochari ya Murang’a.

“Ripoti ya upelelezi inaonyesha kwamba mke wa mshukiwa, Bi Muthoni Gitau, alikuwa amemuacha miezi miwili iliyopita baada ya mzozo wa kinyumbani na akamwachia watoto hao,” akasema Bw Kainga.

Hatimaye, majirani baada ya kuingiwa na shaka za kukosa kuona watoto hao walifanya uchunguzi wao na ndipo juhudi zilizoshirikishwa na chifu wa eneo hilo Bw Jason Hiuhu kuishia kuwapata watoto hao wakiwa wanechinjwa shingoni na kuaga dunia ndani ya nyumba yao.

“Baada ya kuachiwa watoto hao, mshukiwa aliamua kumpeleka wa kwanza kwa shangazi yake na mwingine kwa nyanya yake, lakini wiki mbili zilizopita aliwachukua na kuwarejesha bomani huku ikiaminika aliwachinja asubuhi ya Desemba 20, 2023,” akasema Bw Hiuhu.

  • Tags

You can share this post!

Waislamu mjini Eldoret walaani hatua ya Papa...

Ushoga: Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Kenya wamtetea...

T L