• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Ole wenu mliomtamani, Akothee aoleka na mchumba wake mzungu

Ole wenu mliomtamani, Akothee aoleka na mchumba wake mzungu

NA SAMMY WAWERU

MWANAMUZIKI tajika Esther Akoth maarufu kama Akothee anafanya harusi hii leo, Jumatatu, Aprili 10, 2023.

Bi Akothee anaolewa na mchumba wake, ambaye ni mzungu.

Mwimbaji huyo wa kibao cha Kula Ngoma, amekuwa akipakia picha zake pamoja na kipenzi chake cha moyo kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Amemtambulisha kwa umma, hasa jamii ya wanamitandao kwa jina moja pekee, Bw Schweizer.

Hata hivyo, amembandika jina Omosh – Jina lenye asili ya jamii ya Kijaluo.

Mwanamuziki Esther Akoth almaarufu Akothee. PICHA / HISANI

Harusi yake inahudhuriwa na waliopewa mwaliko pekee, Akothee akionya wenye nia kufuruga siku hii maalum maishani mwake.

“Ninakemea kwa Jina la Yesu mpango wowote wenye nia mbaya,” alisema mnamo Jumamosi.

“Harusi yangu lazima ifanikiwe, kwa sababu mimi ni mtu mwenye roho safi. Na ifahamike, watakaohudhuria lazima wawe na kadi ya mwaliko ambayo mimi mwenyewe, Madam Boss nimeitia Saini,” Akothee, 39, aliambia wanahabari.

Mwimbaji Akothee anafunga pingu za maisha na kipenzi chake Omosh. PICHA / HISANI

Na kwa yeyote mwenye nia kuvuruga sikukuu kufunga pingu za maisha na ‘Omosh’, alisema ajiandae kuaibishwa kupitia mitandaoni.

Akiwa mama wa watoto watatu wazima, Akothee ametoka Kaunti ya Migori na mapema mwaka huu aliongoza ujumbe wa mchumba wake kutembelea wazazi wake.

Kando na kuwa mwimbaji, ni mfanyabiashara ambapo amewekeza katika sekta ya utalii, mashamba na pia ana wakfu kusaidia wasichana wanaotoka familia maskini.

Si mara ya kwanza Akothee, ambaye anajitambua kama ‘Rais wa Singo Matha’, kuchapisha kwenye akaunti zake za mitandao wanaume alio kwenye uhusiano.

  • Tags

You can share this post!

MAPISHI KIKWETU: Jinsi ya kuandaa uduvi almaarufu...

Tabia na mambo ya kuepuka asubuhi

T L