• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 3:13 PM
Rais Ruto asambaza zawadi za Krismasi, wewe umefikiwa?

Rais Ruto asambaza zawadi za Krismasi, wewe umefikiwa?

PCS na CHARLES WASONGA

RAIS William Ruto na Mama wa Taifa Rachel Ruto mnamo Ijumaa walisambaza zawadi za Krismasi kwa wakazi wa eneobunge la Turbo huku wakiwatakia Wakenya Krismasi njema na Mwaka Mpya wa fanaka.

Wawili hao walisambaza vyakula mbalimbali ikiwemo unga wa mahindi, mafuta ya kupikia, unga wa ngano, mchele, sukari miongoni mwa vingine.

Wakati huo huo, Rais Ruto alikariri kujitolea kwa serikali yake kupunguza gharama ya matibabu kupitia sheria za kufanikisha Mpango wa Afya kwa Wote (UHC).

“Chini ya sheria hii, wale raia wasio na ajira ambao wamekuwa wakilipa ada ya Sh500 kwa mwezi kama mchango wa Bima ya Kitaifa ya Afya (NHIF) sasa watalipa Sh300 pekee na kutibiwa maradhi yote ikiwemo kansa,” Rais akaeleza.

Rais alisema ni makosa kwa watu fulani kuenda kortini kusitisha miradi inayolenga kuimarisha maisha ya Wakenya kama vile mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu.

“Chini ya mpango wa ujenzi wa nyumba, nyumba 200,000 zitajengwa kila mwaka. Kufikia sasa, zaidi ya watu 12,000 wameajiriwa katika maeneo 31 kunakojengwa nyumba hizo,” akasema Rais Ruto.

  • Tags

You can share this post!

Balala ashtakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi

Rais Samia Suluhu avunja bodi ya Tanesco kufuatia kupotea...

T L