NA KEVIN CHERUIYOT
VIONGOZI wa Azimio La Umoja-One Kenya wakiongozwa na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, Tim Wanyonyi (Westlands) na Babu Owino (Embakasi Mashariki), wamewatembelea wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kihumbuini.
Ziara yao inajiri siku mbili baada ya watoto hao kurushiwa gesi ya kuwatoa machozi wakati wa maandamano yaliyofanyika mnamo Jumatano wiki hii.
Kiongozi wa Azimio Raila Odinga aliitisha maandamano na kuwahimiza Wakenya wajitokeze kwa wingi kupinga hatua ya serikali ya Kenya Kwanza kuleta ushuru mpya ambao anasema utafanya gharama ya maisha kuendelea kupanda.