• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 5:55 AM
Viongozi wa Azimio wawatembelea wanafunzi waliorushiwa ‘tear gas’

Viongozi wa Azimio wawatembelea wanafunzi waliorushiwa ‘tear gas’

NA KEVIN CHERUIYOT

VIONGOZI wa Azimio La Umoja-One Kenya wakiongozwa na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, Tim Wanyonyi (Westlands) na Babu Owino (Embakasi Mashariki), wamewatembelea wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kihumbuini.

Ziara yao inajiri siku mbili baada ya watoto hao kurushiwa gesi ya kuwatoa machozi wakati wa maandamano yaliyofanyika mnamo Jumatano wiki hii.

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga aliitisha maandamano na kuwahimiza Wakenya wajitokeze kwa wingi kupinga hatua ya serikali ya Kenya Kwanza kuleta ushuru mpya ambao anasema utafanya gharama ya maisha kuendelea kupanda.

  • Tags

You can share this post!

Walioshtakiwa kwa kashfa ya Sh3.5 bilioni ya Anglo Leasing...

Maandamano ya Azimio kufanyika siku tatu kila wiki

T L