• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 4:26 PM
81 wanyongwa nchini Saudia

81 wanyongwa nchini Saudia

NA MASHIRIKA

RIYADH, SAUDI ARABIA

SAUDI Arabia Jumamosi iliwanyonga watu 81, hiyo ikiwa idadi kubwa kuliko watu walionyongwa mwaka 2021.

Watu hao—waliojumuisha raia saba kutoka Yemen na mmoja kutoka Syria— walihukumiwa kwa “makosa tofauti” baadhi yakiwa kushiriki kwenye vitendo vya kigaidi, kulingana na kituo cha habari cha serikali, SPA.

Baadhi ya watu hao walihukumiwa kwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi la Islamic State (IS).

Wakati huo huo, mwanablogu aliyefungwa gerezani kwa miaka kumi “kuikosoa dini ya Kiislamu” aliachiliwa huru Jumamosi.

You can share this post!

Matumaini tele utalii kupigwa jeki

WANDERI KAMAU: Wanahabari waangazie wagombeaji kwa usawa

T L