NA MASHIRIKA
RIYADH, SAUDI ARABIA
SAUDI Arabia Jumamosi iliwanyonga watu 81, hiyo ikiwa idadi kubwa kuliko watu walionyongwa mwaka 2021.
Watu hao—waliojumuisha raia saba kutoka Yemen na mmoja kutoka Syria— walihukumiwa kwa “makosa tofauti” baadhi yakiwa kushiriki kwenye vitendo vya kigaidi, kulingana na kituo cha habari cha serikali, SPA.
Baadhi ya watu hao walihukumiwa kwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi la Islamic State (IS).
Wakati huo huo, mwanablogu aliyefungwa gerezani kwa miaka kumi “kuikosoa dini ya Kiislamu” aliachiliwa huru Jumamosi.