MASHIRIKA Na CHARLES WASONGA
TAARIFA iliyotolewa jioni na Wizara ya Masuala ya Ndani ya Morocco inasema kuwa watu 1,037 wamethibitishwa kufa kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea nchini humo Ijumaa usiku.
“Aidha, jumla ya watu 1,204 wamejeruhiwa, 721 miongoni mwao wakiwa hali mahututi,” taarifa kutoka kwa wizara hiyo ikaongeza.
Tetemeko la kiwango cha 6.8 kwa kipimo cha Richter lilisababisha uharibifu mkubwa nchini humo, raia na watalii wakilazimika kutorokea maeneo salama Ijumaa usiku na Jumamosi.