• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Idadi ya waliopoteza maisha kwenye tetemeko la ardhi nchini Morocco yafika 1,037

Idadi ya waliopoteza maisha kwenye tetemeko la ardhi nchini Morocco yafika 1,037

MASHIRIKA Na CHARLES WASONGA

TAARIFA iliyotolewa jioni na Wizara ya Masuala ya Ndani ya Morocco inasema kuwa watu 1,037 wamethibitishwa kufa kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea nchini humo Ijumaa usiku.

“Aidha, jumla ya watu 1,204 wamejeruhiwa, 721 miongoni mwao wakiwa hali mahututi,” taarifa kutoka kwa wizara hiyo ikaongeza.

Tetemeko la kiwango cha 6.8 kwa kipimo cha Richter lilisababisha uharibifu mkubwa nchini humo, raia na watalii wakilazimika kutorokea maeneo salama Ijumaa usiku na Jumamosi.

  • Tags

You can share this post!

Nondies, Kabras na KCB waingia 8-bora katika duru ya...

Mhandisi ajeruhiwa baada ya gari kukanyaga kilipuzi katika...

T L