Na MASHIRIKA
ALBANY, NEW YORK
RAIS wa zamani wa Amerika, Donald Trump, amejitetea akidai kuwa hatua ya kumshtaki inalenga kuhujumu azma yake ya kuwania kiti cha urais mwaka 2024.
Rais huyo wa zamani alifikishwa mahakamani kwa mashtaka ya kumlipa mwanamke mmoja nyota wa filamu za ngono kabla ya uchaguzi ili kumnyamazisha asitoboe siri.
Trump amewakosoa waendesha mashtaka nchini humo akisema “wanakiuka Sheria ya nchi hiyo.”
Subscribe our newsletter to stay updated