• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Rais Jammeh kushtakiwa kwa utawala mbovu

Rais Jammeh kushtakiwa kwa utawala mbovu

NA AFP

BANJUL

SERIKALI ya Gambia imemfungulia mashtaka ya mauaji rais wa zamani wa nchi hiyo Yahya Jammeh kulingana na mapendekezo ya tume ya ukweli na maridhiano.

Tume hiyo ilipendekeza kuwa Jammeh anastahili kufunguliwa mashtaka ya mauaji na makosa mengine ya uhalifu wakati alipokuwa madarakani kati ya 1994 na 2017.

Tume hiyo huru ilisema Jammeh na watu aliokuwa nao serikalini, walihusika nkatika makosa 44 ya uhalifu yakiwemo mauaji na unajisi, dhidi ya waandishi wa habari, wanajeshi, na upinzani.

  • Tags

You can share this post!

Waziri atimuliwa baada ya watoto 11 kuteketea

EACC yaandama Sh1.9 bilioni za Waititu

T L