NA MASHIRIKA
DAR ES SALAAM, TANZANIA
NAIBU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Tundu Lissu, amesema serikali ya Tanzania imemlipa kiinua mgongo aliochukuwa akidai kwa kuhudumu kama mbunge kwa zaidi ya miaka mitatu.
Lissu, ambaye sasa anaishi nchini Ubelgiji, alipokonywa ubunge mwaka 2019 kwa sababu ya kuishi ughaibuni kwa muda mrefu akipokea matibabu maalum, baada ya kumiminiwa risasi 16 na watu wasiojulikana mnamo 2017.
Lissu alimtaka Rais Samia Suluhu Hassan kumlipa marupurupu hayo wawili hao walipokutana nchini Ubelgiji Februari 2022.