• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
Rais wa zamani Da Silva ashinda tena urais Brazil

Rais wa zamani Da Silva ashinda tena urais Brazil

NA MASHIRIKA

SAO PAULO, BRAZIL

ALIYEKUWA rais wa Brazil, Lula da Silva, ameibuka mshindi kwenye uchaguzi wenye ushindani mkali, uliofanyika nchini humo Jumapili.

Hata hivyo, Lula alishinda kwa kukaribiana sana na rais wa sasa, Jair Bolsonaro. Lula alizoa asilimia 50.8 ya kura, huku Bolsonaro akizoa asilimia 49.2.

Kufikia jana Jumatatu, Bolsonaro hakuwa ametoa taarifa yoyote kukubali matokeo hayo. Wadadisi wanatabiri kuwa kuna uwezekano akayakataa.

“Leo, mshindi wa pekee ni raia wa Brazil,” akasema Da Silva, alipohutubia maelfu ya wafuasi wake jijini Sao Paulo.

  • Tags

You can share this post!

Achani ateua mawaziri wapya, adumisha 4 pekee wa Mvurya

Mikakati ya UDA kumaliza Kalonzo

T L