NA MASHIRIKA
WATU 9 milioni hufa kila mwaka kote duniani kutokana na uchafuzi wa mazingira, utafiti mpya unaonyesha.
Utafiti uliofanywa na wanasayansi na ripoti yake kuchapishwa katika jarida la Lancet unaonyesha kuwa mazingira huchafuliwa na shughuli za kibinadamu ikiwemo viwanda, na mataifa yaliyostawi kiviwanda ndiyo huathirika zaidi.
India na China zinaongoza duniani kwa vifo vitokanavyo na uchafuzi wa mazingira, karibu vifo 2.4m hadi vifo 2.2m kwa mwaka, ingawa mataifa hayo pia yana idadi kubwa ya watu duniani.