• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:09 PM
Wanawake waandamana kupinga agizo la kufungwa kwa saluni

Wanawake waandamana kupinga agizo la kufungwa kwa saluni

Na AFP

KABUL, Afghanistan

MAAFISA wa Usalama walifyatua risasi hewani na kutumia gesi za kuwafanya watu kutoa machozi ili kuwatawanya wanawake waliokuwa wakiandamana jijini Kabul kupinga amri ya utawala wa Taliban kuzima biashara za saluni.

Hiyo ni hatua ya hivi punde ya kudhibiti uhuru na haki za wanawake na wasichana nchini humo.

Tangu ulipotwaa mamlaka Agosti 2021, utawala wa Taliban umepiga marufuku wasichana na wanawake kuhudhuria shule na vyuo vikuu.

Aidha, wamezimwa kujivinjari katika maeneo ya starehe, vituo vya kufanya mazoezi ya viungo na kuamriwa kufunika nyuso zao katika maeneo ya umma.

Tafsiri: CHARLES WASONGA

  • Tags

You can share this post!

Wandayi asema Raila yuko salama licha ya kutoonekana...

Maafisa watibua njama ya wahuni kuteketeza kituo cha polisi

T L