Na AFP
KABUL, Afghanistan
MAAFISA wa Usalama walifyatua risasi hewani na kutumia gesi za kuwafanya watu kutoa machozi ili kuwatawanya wanawake waliokuwa wakiandamana jijini Kabul kupinga amri ya utawala wa Taliban kuzima biashara za saluni.
Hiyo ni hatua ya hivi punde ya kudhibiti uhuru na haki za wanawake na wasichana nchini humo.
Tangu ulipotwaa mamlaka Agosti 2021, utawala wa Taliban umepiga marufuku wasichana na wanawake kuhudhuria shule na vyuo vikuu.
Aidha, wamezimwa kujivinjari katika maeneo ya starehe, vituo vya kufanya mazoezi ya viungo na kuamriwa kufunika nyuso zao katika maeneo ya umma.
Tafsiri: CHARLES WASONGA