• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Ndoa ya mitara inatambulika kisheria, Karen Nyamu ajitetea ‘akihalalisha’ penzi lake kwa Samidoh

Ndoa ya mitara inatambulika kisheria, Karen Nyamu ajitetea ‘akihalalisha’ penzi lake kwa Samidoh

NA FRIDAH OKACHI

SENETA Maalum Karen Nyamu ametetea uhusiano wake na mwanamuziki Sammy Muchoki almaarufu Samidoh.

Wawili hao wana watoto wawili.

Kwenye mahojiano na mwanahabari Fredrick Muitiriri mnamo Oktoba 9, 2023, Bi Nyamu alionekana kukerwa na maswali kuhusu uhusiano wake na Samidoh, akijibu kuwa hajavunja sheria yoyote.

“Sasa, ni mimi peke yangu ninayeweka familia mitandaoni? Hujawahi kuona familia ya Rais mitandaoni? Hilo ni swali gani? Hilo swali si sawa. Unajua sheria za Kenya vizuri? Nenda uangalie sheria ya ndoa ya zaidi ya mke mmoja ambayo ilipitishwa na bunge. Sijavunja sheria mimi. Kuna watoto wanaohusika na sidhani hayo ndio maswali yalinileta hapa,” alijibu Bi Nyamu.

Mwanahabari Muitiriri aliendelea kuuliza mwanasiasa huyo iwapo anaamini kuwa ni kielelezo bora kwa vijana hapa nchini.

“Mimi nafuata sheria. Sheria haijatengezewa nyani na ninaifuata. Mimi naishi maisha ya kiuhalisia bila kujifanya. Vijana waige hivyo na wasiogope. Ima iwe ni familia, kazi, na hata biashara, au maono na ndoto, fanya uamuzi bora kuhusu maisha yako. Usiangalie mwenzako ambaye hajali,” aliongezea kiongozi huyo.

Bi Nyamu amekuwa akisisitiza kuwa hali aliyomo si rahisi kwa watoto kuhusishwa.

Seneta huyo maalum alisema kuingia kwa mahusiano kila wakati huwa na ugumu wake na wakati mwingine husababisha mtu kuumizwa kihisia iwapo hatashughulikia suala hilo kwa uangalifu.

Mwanamuziki wa mtindo wa Mugithii Bw Samidoh ana watoto wengine watatu na mke wake Edday Nderitu, ambaye aliondoka nchini na kuhamia nchini Marekani. Hali hii imefanya wengi wahisi ndoa hiyo iliyumba.

  • Tags

You can share this post!

Visa vya moto, migomo vyaongezeka katika shule za Ganze...

Utamaduni Dei: Taswira mseto mahasla wakifungua biashara...

T L