• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:55 AM
Pasta Ng’ang’a asema makataa yake yamesaidia wengi kutafuta wachumba tayari kwa ndoa

Pasta Ng’ang’a asema makataa yake yamesaidia wengi kutafuta wachumba tayari kwa ndoa

NA MERCY KOSKEI

MCHUNGAJI wa Kanisa la Neno Evangelism James Maina Ng’ang’a amedai kuwa waumini wa kanisa lake ambao wamekuwa ‘singo’, wameanza kufanya mipango ya harusi tangu alipotoa makataa ya miezi sita kuwahimiza kutafuta wachumba na kufunga ndoa.

Mnamo Jumapili, Novemba 6, 2023, mhubiri huyo alithibitisha kwamba kwa sasa washirika watatu tayari wamemdokezea kuhusu mipango yao ya kutaka kuanza maisha ya ndoa na kuanzisha familia na wachumba wao.

Wiki mbili zilizopita, video ya Ng’ang’a ilisambaa mitandaoni baada ya kutoa ‘ultimatum’ ya miezi sita kwa washirika wa kanisa lake wapate wachumba.

Ng’ang’a aliendelea kwa kuwaambia waumini katika kanisa hilo wakome kutumia visingizio na kulaumu ama ‘mubaba na mumama‘ kwa kuiba wapenzi wao.

Hata hivyo, katika video mpya iliyochapishwa Ng’ang’a alijigamba jinsi agizo lake sasa linavyosaidia wengi kuanza kufikiria kujitafutia wachumba.

“Najua nawaambia watu ninaowafahamu kwa sababu sitaki wapoteze muda bila kuoa au kuolewa. Tangu niseme hivyo, watu watatu wameanza mipango hiyo, watatu hao wamenieleza kuwa wana wachumba na ama wanataka kuolewa au kuoa,” alisema.

Amesema makataa aliyotoa yamepokelewa kwa hisia mseto lakini hajali kwani “nia yangu ni kuwasaidia watu”.

Alitetea hatua yake ya kupeana makataa akisema kuwa alikuwa anawapa watoto wake wa kiroho (waumini) mawaidha kwani ni baba yao wa kiroho.

“Makataa niliyopeana ni kwa watoto wangu wa kiroho. Kwa nini nikuweke hapa na hufurahii maisha yako? Mimi naongea na wale ambao wako kwangu… wale nimepewa niwaongoze. Sitaki kuona mtu akitangatanga… nataka kuona mtu akiwa kwake na familia yake,” alisikika akishauri.

Wafuasi wake mitandaoni walifurika kwenye safu ya maoni, kutoa hisia zao tofauti kutokana na ujumbe wake.

“Ushauri mzuri kutoka kwa baba mwenye upendo, neema zaidi papa,”  akaandika Monicah Muthoni.

“Ndio pasta, wewe ni baba anayewajibika bila shaka,” akasema Glado39.

  • Tags

You can share this post!

Wafanyabiashara mjini Kilifi wakerwa kufurushwa bila...

Jinsi waziri Kuria alivyojipalia makaa kwa kumtetea Mwangaza

T L