Mpendwa Daktari,
Homa ya mapafu (Nimonia) husambaa vipi?
Irene, Nairobi
Mpendwa Irene,
Nimonia ni ugonjwa unaoathiri moja au mapafu yote na husababishwa na bakteria, virusi au ukuvu.
Kuna aina ya nimonia inayosambazwa kupitia matone yaliyo viumbehai vinavyosababisha ugonjwa huu. Viumbehai hivi huingia kwenye hewa wakati mtu aliyeambukizwa anapopiga chafya au kukohoa.
Wakati mwingine maradhi haya hutokea wakati baadhi ya bakteria na virusi vinavyopatikana mdomoni, kooni na puani, vinapoingia kwenye mapafu.
Ni kawaida kwa mtu kuondoa uowevu ulio na virusi hivi kutoka mdomoni, puani na kooni lakini kama kawaida mfumo wa kinga mwilini huwa na uwezo wa kupigana navyo.
Lakini, iwapo hali ya kiafya ya mhusika imedhoofika kutokana na maradhi mengine, basi huenda akashambuliwa na aina kali ya ugonjwa huu.
Watu ambao hapo awali walishambuliwa na virusi, ugonjwa wa mapafu, maradhi ya moyo na kooni vilevile wanaotumia pombe na dawa za kulevya, wamo katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa huu.
Ishara za Nimonia
Ugonjwa huu huthibitishwa vipi?