• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:55 AM
DOMO KAYA: Wanaume twakwama wapi?

DOMO KAYA: Wanaume twakwama wapi?

Na MWANAMIPASHO

AISEE! Sijui leo nianzie wapi.

Wanaume hivi tunakwama wapi? Mwanzo kuna huyu Samidoh, eti kampachika ujauzito mwingine Karen Nyamu. Mimba ina miezi mitatu. Nipo hapa mwenzako nashangaa, yaani demu hata bado hajapona vizuri ushapanda mbegu nyingine! Jamani si ni juzi tu totos kakuzalia?

Hivi si ni miezi sita imepita toka umwombe mkeo msamaha kwa kumshusha Karen rinda na kumjaza kiumbe? Nashindwa kupata picha kabisa, mwenzako si bado atakuwa ananyonyesha ukizingatia alijifungua Disemba 2020? Leo ana kiumbe mwingine.Itakuwa ni mimi sielewi Samidoh anakwama wapi au itakuwa Karen ni mtamu ajabu. Au pengine Samidoh anayapenda madrama ya Karen sababu wapo wanaume wa dizaini hii. Nasema hivi sababu alikuwepo jamaa kabla ya Samidoh na huyo bwana ambaye ni DJ, alikiri waziwazi kuwa madrama ya Karen ndiyo yalimfanya amalize uhusiano wao.

Mweeh! Sielewi.Ila subiri kidogo, unajua nilikuwa nimeisahau hili jipya la huyu askofu wa kanisa la House of Grace David Murithii.

‘Mtumishi wa Mungu’ au ukipenda mwite ‘mtumishi wa uchu’, baada ya kukwepa kwepa ile stori ya kumla ‘kondoo’ wake sasa kakiri ni kweli alivunja amri ya sita kwenye Biblia.

Murithii kakiri kweli alikagua mali ya binti wa watu na kumpachika mimba. Kabla hata sijaenda mbali, huyu ni muhubiri ambaye kila Jumapili yupo madhabahuni akikuletea neno la Mungu.

Lakini bado jamaa alimfanyia Mungu u -mafia kwa kuvunja amri ya sita ya mafundisho yake anayoyafahamu vizuri sana. Badala azingatie kulishana neno, mubaba aliamua pia alishane nondo.

Angalikuwa singo ningalimwelewa ila jamaa amedumu kwenye ndoa na mkewe Ronica kwa miaka 31 sasa.

Mamangu husema, mwanamume hufa na nguvu zake ila mwanamke kadri miaka inavyoongezeka ndivyo naye anavyozidi kuchujuka, anaisha mvuto na ladha.

Hivi inawezekana ndio sababu Murithii aliamua kumwendea totos bila kuwazia yanayoweza kutokea baadaye?

Lakini kama haitoshi, kilichonichokesha zaidi ni pale mubaba alivyosema kwamba, pamoja na kukiri kumzalisha totos mtoto wa kiume, yupo tayari kutoa matunzo ya kila mwezi lakini uwezo wake sio mkubwa.

Askofu-fisi kaiambia mahakama uwezo wake wa kutoa malezi ya kila mwezi ni Sh10,000 pekee na wala hana uwezo wa kutoa Sh100,000 anazodai msupa huyo.

Mume wa mtu kadai yeye ni maskini, na kwamba anategemea michango kutoka kwa wahisani ili kuishi. Huyu bwana ana mchezo.

Hivi ni nani asiyejua makanisa ni biashara kubwa ya mamilioni ya pesa katika taifa hili? Ndio sababu Rais Paul Kagame alipiga marufuku kufunguliwa kwa makanisa mapya Rwanda.

Murithii ana zaidi ya matawi matatu ya kanisa lake Mombasa, Nairobi na kwingineko.

Hivi alipokuwa akipata utamu wa totos badala ya mkewe, hakujua yeye ni maskini?

Halafu sasa kuna hii ya mtangazaji wa Citizen Trevor Ombija. Kumbe jamaa sio mpigaji mbinja mzuri. Ndugu yangu kwa sauti yako nzito, umaarufu, kimo na mwili uliochongwa vilivyo kutokana na zile shughuli za gym, unawezaje kumchumbia mwanamke miaka 10, ukapeleka mahari kisha akakutema?

Kinachonisikitisha zaidi ni kuwa kwa miaka hiyo huna lolote la kuonyesha kutoka kwenye uhusiano huo. Ulichovya asali miaka kumi lakini hata kuacha muhuri kwa kumzalisha binti wa watu ulishindwa.

Hivi mazoezi unayokeshea gym yanakufaidi nini zaidi ya kukuchongeshea mwili?

Mimi nilifikiri watu wa dizaini yako hamuwezi kupigwa ‘character development’.

Hivi hujui wewe ni toto-shoo?

Leo ukitangaza unataka demu, naamini hata trela mbili watajaza na wabaki.

Kaka mbona miaka yote hiyo 10 inaniuma? Hawa watoto wazuri wengine huwa unawaona? Au huyo alikufanyia anachodaiwa kuwafanyia wanaume wa watu soshiolaiti Amber Ray.

Amber wanasema akimshika mumeo, kisha apange safari ya kwenda kwao Ukambani kule Kitui au sijui ni Machakos, ndio basi humuachi. Atakuacha yeye akichoka au akimpata ‘potential’ mwingine.

Aisee, Trevor kwa levo yako wewe sio mwanamume wa kupigwa ‘character development’!

You can share this post!

Kane abeba Spurs hadi hatua ya makundi ya Europa Conference...

Raila amtaka Mutyambai asafishe polisi kuondoa uozo