• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 8:50 AM
Faida za matomoko kiafya

Faida za matomoko kiafya

NA MARGARET MAINA

[email protected]

MATOMOKO ni tunda la kijani kibichi, lenye umbo la koni na hukuzwa sana katika maeneo ya tropiki.

Mara nyingi huliwa kwa kijiko. Kwa kawaida huwa na ladha tamu sawa na matunda mengine ya kitropiki, kama vile ndizi na nanasi.

Kwa wingi wa nyuzi, vitamini, na madini, tunda hili la kipekee linaweza kukupa kinga, kupunguza uvimbe, na kukuza afya ya macho na moyo.

Matomoko ni chanzo bora cha vitamini B6

Vitamini B6 ina jukumu muhimu katika kuundwa kwa nyurotransmita, ikiwa ni pamoja na serotonini na dopamine, ambazo husaidia kudhibiti hisia zako. Viwango visivyotosha vya vitamini hii vinaweza kuchangia shida za mhemko.

Viwango vya chini vya vitamini B6 vinahusishwa na unyogovu, hasa kwa wazee.

Kuzuia shinikizo la damu

Matomoko yana virutubisho vingi vinavyosaidia kudhibiti shinikizo la damu, kama vile potasiamu na magnesiamu.

Potasiamu na magnesiamu huchangia upanuzi wa mishipa ya damu, ambayo husaidia kupunguza shinikizo la damu. Shinikizo la damu linaweza kuongeza hatari yako ya kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo na kiharusi.

Usagaji mzuri wa chakula

Kwa sababu nyuzinyuzi haziwezi kuyeyushwa au kufyonzwa, tunda la matomoko lina nyuzinyuzi nyingi ambazo zinaweza kulisha bakteria wazuri kwenye utumbo wako, na kusaidia kwa mmeng’eyo mzuri wa chakula.

Kingamwili

Matomoko ni chanzo kikubwa cha Vitamini C, kirutubisho kinachoboresha kinga na kulinda dhidi ya magonjwa. Upungufu wake husababisha hatari kubwa ya kupata maambukizi. Vitamini C inaweza kusaidia katika kupunguza muda wa homa ya kawaida.

Kukabili ugonjwa wa baridi yabisi

Wakati asidi inapowekwa kwenye viungo, husababisha ugonjwa wa yabisi. Magnesiamu, ambayo hupatikana kwa wingi kwenye matomoko, huweka usawa wa maji mwilini na hivyo kusaidia katika kutoa asidi kwenye viungo. Pia hutoa nguvu kwa misuli.

  • Tags

You can share this post!

Kwinoa na faida zake kwa binadamu

Mivutano yatishia hesabu za Ruto eneo la Magharibi

T L