FASIHI SIMULIZI: Udhaifu wa mbinu za ukusanyaji data
JUMA lililopita, tuliangazia umuhimu wa mbinu za ukusanyaji data ya Fasihi Simulizi.
Leo tutajadili udhaifu wa mbinu zizo hizo kwa manufaa ya mtafiti.
MAHOJIANO
Udhaifu
- Ni mbinu inayohitaji muda mrefu kwani mtafiti na mtafitiwa hutumia wakati mwingi kukutana ana kwa ana.
- Mhojiwa anaweza kutoa habari za uwongo kwa sababu hawajuani.Kikwazo cha mawasiliano iwapo watafitiwa au jamii lengwa haijui kusoma na kuandika.
- Ni mbinu ghali kutokana na gharama ya usafiri ikiwa walengwa ni wa mbali.
- Ufisadi – wahojiwa wakati mwingine huitisha mlungula/hongo kabla ya kukubali kushiriki katika mahojiano.
KUTAZAMA/UTAZAMAJI
Udhaifu
- Hata kama huhitaji kitendo cha kutazama tu, mawasiliano yaweza kuwa kikwazo iwapo mtafiti hafahamu lugha ya watafitiwa.
- Ukosefu wa uaminifu humfanya mtafitiwa kukosa kutoa ujumbe wa kweli.
- Ni ghali kwa sababu mtafiti lazima asafiri hadi nyanjani mwa watafitiwa.
KUREKODI KATIKA KANDA ZA SAUTI/TEPUREKODA/VIDEO/FILAMU
- Nguvu za umeme zinaweza kukosekana/kutoweka hivyo utafiti kuathiriwa.
- Vifaa hivi haviwezi kunasa hisia, viziada lugha na uigizaji kwa jumla.
- Fanani anaweza kuupiga chuku uwasilishaji wake hata kupoteza ujumbe kwa sababu anajua kuwa anarekodiwa.
- Ni mbinu ghali kwani mtafiti anahitaji kununua kifaa na kumbidi mtafiti kusafiri.
HOJAJI
Udhaifu wa Hojaji
- Kunaweza kutokea utata wa maswali na hivyo kusababisha majibu yasiyo sahihi.
- Wasiojua kusoma na kuandika hawatatumia mbinu hii
- Itakuwa vigumu kupata sifa za uwasilishaji kama vile kiimbo, toni na ishara/viziada lugha.
- Wahojiwa wanaweza kukataa kuijaza kutokana na mwelekeo hasi dhidi ya hojaji na hivyo kukwamiza utafiti.
Kipkoros Borwo
Alliance Girls High School
Next article
Wanasiasa wasukumwa kueleza mipango ya kuinua utalii