• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
HUKU USWAHILINI: Leo nakupasha ya Andunje, mfupi wa kimo ila kwa makeke ni noma!

HUKU USWAHILINI: Leo nakupasha ya Andunje, mfupi wa kimo ila kwa makeke ni noma!

NA SIZARINA HAMISI

KAWAIDA wanawake wengi huwa na matarajio na mtazamo wa mwanamume ambaye anafaa kuwa kwenye uhusiano.

Nao wengi hupenda kutaja awe mrefu ikiwa ni mojawapo ya kigezo cha mvuto.

Lakini huku kwetu Uswahilini, wanaume wafupi ndio wanasakwa na wengi na sababu ni kwamba wanajua kujinadi na kujieleza ujuzi na mbinu zao katika suala la mahaba.

Mfano ni huyu kaka tunayemuita Andunje ambaye ni mfupi wa kutosha lakini ana makeke kiasi kwamba mtaa mzima anajulikana.

Wiki iliyopita alituacha midomo wazi alipoamua kumchamba msichana mmoja aliyejaribu kumdhalilisha sababu ya kimo chake.

Tena mazungumzo yake na huyo msichana alihakikisha yanafanyika eneo la wazi, pale ambapo washambenga wa mtaa wanaketi ili nao pia wasikie yale aliyoamua kutiririka siku hiyo.

Bila ajizi, Andunje akamwambia kwamba yule mwanamume aliyekuwa mpenzi wake anatembea pia na rafiki yake, kwamba huo urefu wa huyo jamaa unamtamanisha kwa wanawake wengine, na yeye hajali wala nini, anaendelea kutafuna huku na kule.

Akamwambia yeye akipenda mahali anatulia bila hofu ya kulaghaiwa, aje kwake kwani wengi hawavutiwi na kimo chake.

Akaendelea kumvurumishia maneno kwamba yeye ni hodari sana katika sekta ya kufanya mapenzi, habahatishi na tena anajua na kuelewa shughuli kiasi kwamba hao wanaume warefu hawamfikii hata robo.

Washambenga wa Uswahilini tukatega masikio vizuri, mzee wa kimo kifupi akiendelea kujimiminia sifa zake, kwamba kwake uvumilivu ni nguzo ya mapenzi, tena akamwambia akimuoa awe na uhakika atadumu naye kwani ana uwezo wa kuvumilia mengi ambayo hao wanaume warefu ni nadra kuyavumilia.

Tena akamwambia atapumzika kuvaa viatu vyake virefu katika jitihada za kufikia kimo cha mpenzi wake mrefu.

Akamdokeza kwamba akitoka naye usiku hana haja ya kuvaa viatu virefu kwani ameona jinsi anavyohangaika navyo akitembea kama vile anaruka vidimbwi vya maji.

Kwa kumalizia bwana Andunje akamwambia kwamba hicho kimo chake kisimhadae, kwani ni muonekano wa nje na kwamba akifungua maeneo mengine atapigwa na butwaa jinsi alivyosheheni bidhaa muhimu.

Sasa hii kauli yake ya mwisho ndio ambayo imemuundia soko jipya kwa mashambenga wa hapa mtaani, kwani nawajua wanawake kadhaa ambao hivi sasa wako tayari kufunguliwa maeneo mengine ili waone hizo bidhaa zilizosheheni na ikibidi wazifanyie majaribio.

[email protected]

You can share this post!

7 wauawa katika mapigano Sudan

SHANGAZI SIZARINA: Nina wasiwasi kumhusu binti yangu,...

T L